Baraza la mawaziri jipya...holoo


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898 
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz 

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

MAWAZIRI


1. OFISI YA RAIS


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,


2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H. Suluhu, Mb.,


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,


3. OFISI YA WAZIRI MKUU


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,


4. WIZARA


Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,


Waziri wa Ujenzi
Dr. John P. Magufuli, Mb.,


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,


Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,


Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,


Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,


Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame M. Mbarawa, Mb.,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,


Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,
 Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,
Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,


Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,


Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,


Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,
5. NAIBU MAWAZIRI


OFISI YA RAIS
HAKUNA NAIBU WAZIRI


6. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,


7. OFISI YA WAZIRI MKUU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,


8. WIZARA MBALIMBALI
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,


Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,


Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,


Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,


Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,


Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,


Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro NyalanduMb.,
Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson LwengeMb.,


Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman RashidMb.,


Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,


Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,


Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,


Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,


Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith MahengeMb.,


Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,


Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,


Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,


Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,


Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
Mei, 2012

Rich Mavoko ndani ya mbeya city


Mkali wa mavoko toka Dar es salaam... sasa anakuja mbeya live kwenye kumsaka kimwana mrembo wa Mbeya city yaani KATIKA SHINDANO  LA KUMSAKA MISS MBEYA CITY CENTER, usikose siku hiyooo. Ambayo itakuwa siku ya ijumaa tar 4/5/2012 Kwa kiingilio cha shilingi 10000/- tu! 

Bungeni jingine laibuka ni zito zaidiiii

Bungeni Dodoma

BUNGE la Muungano lililomaliza kikao chake cha kumi jana, lilitikisika baada ya kuibuka kwa tuhuma nyingine nzito zilizoelekezwa moja kwa moja kwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, na naibu wake, Adamu Malima, na Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.
Wakati Ngeleja akishambuliwa kwa kusema uongo na kuficha ufisadi wa kutisha wa ubinafsishaji, Waziri Maige amekaangwa kwa tuhuma za kujihusisha katika ugawaji vitalu vya uwindaji kinyume na sheria.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James lembeli, ndiye aliyeibua tuhuma hizo nzito, kiasi cha kuitaka serikali kumwajibisha waziri huyo, hatua ambayo imezidi kuonyesha uozo wa utendaji ndani ya serikali.
Lembeli akiwasilisha taarifa kuhusu utekelezaji wa shughuli zake katika kipindi cha Aprili, 2011 hadi Aprili 2012, alisema uchunguzi wa kamati hiyo umebaini mchakato wa ugawaji vitalu ulikuwa na dosari nyingi ikiwamo waziri kutangaza majina ya waliopatiwa vitalu bila kuonyesha ni vitalu gani na vingapi walivyopewa.
Alisema baadhi ya kampuni ziligawawa vitalu kinyume na sheria na ushauri wa kamati ya kumshauri waziri kulingana na sifa na vigezo ikiwamo makampuni matatu, Mwanauta and company Ltd, Saidi Kawawa Hunting Ltd na Malagalasi Hunting Safaris Ltd kugawiwa vitalu bila kuwa na sifa.
Lembeli alisema kamati ilibani kampuni 16 ziligawiwa vitalu vya daraja la kwanza na la pili ambavyo havikuombwa wakati kulikuwa na kampuni za kizalendo zilizokuwa na vigezo.
“Dosari hizi ziliathiri dhana ya uwazi na utawala bora, na kuashiria kuwapo kwa rushwa katika zoezi hilo na hivyo kusababisha malalamiko makubwa kutoka kwa waombaji.
“Kamati ya Bunge inapendekeza kwamba Bunge liitake serikali kumwajibisha Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, kwa kutengeneza mazingira ya rushwa ikiwa ni pamoja na kuyanyang’anya makampuni 16 vitalu vilivyogawiwa,” alisema.
Kuhusu usafirishaji wanyama nje bila kufuata taratibu, Lembeli alisema kamati hiyo imependekeza Bunge liiagize serikali kuwachukulia hatua kali za kinidhamu, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Ladislaus Komba, na wale wote waliohusika na utoaji wa vibali hivyo.
Aliitaja kampuni ya Jungle International kuwa moja ya zilizopewa leseni wakati kwa mujibu wa taarifa za Msajili wa Makampuni (BRELA), haipo kihalali na wala haikupeleka maombi ya kupewa wanyama hao.
Alisema waligundua kuwa kibali alichopewa Jungle International kilielezea ukamataji wa wanyama kufanyika katika wilaya za Longido, Simanjiro na Monduli, jambo ambalo ni kinyume na kanuni, kwani kibali lazima kiainishe wilaya moja.
Aidha alisema kampuni ya Jungle si kampuni halali ya kuendesha biashara ya wanyamapori, kwani Desemba 28, 2001 ilibadili jina la shughuli zake na kwa sasa imesajiliwa kwa jina la Jungle Auctioneers & Brokers Company ambayo inafanya shughuli za udalali.
“Kwa msingi huo, wizara kupitia barua kumbukumbu namba GD/T.80/85/98 ya Aprili 29, 2011 iliyosainiwa na M. Madehele kwa niaba ya Katibu Mkuu ilitoa kibali kwa kampuni ambayo haipo. Hali hiyo inadhihirisha udanyanyifu wa kutisha, harufu ya rushwa na uhujumu uchumi wa nchi,” alisema.
Aidha kamati hiyo imebaini kuwa Kamran Ahmed, raia wa Pakistan ambaye mwaka 2009 alijitambulisha kwenye Idara ya Wanyamapori kama mwakilishi wa Serikali ya Jiji la Karachi aliingia mkataba na aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Erasmus Tarimo kwa niaba ya serikali na kusafirisha tembo wanne kinyume cha sheria.
Alisema kamati hiyo ilifanya uchunguzi zaidi na kubaini Julai 19, 2010, wizara hiyo ilitoa kibali kilichosainiwa na B.M.C.M Midala kwa niaba ya serikali ya Katibu Mkuu wa Serikali ya Jiji la Karachi kuruhusu usafirishwaji wa twiga wawili, viboko (2), greater kudu (2) na errands (4).
“Kwa ushahidi uliopo katika kikosi dhidi ya majangili, Arusha, raia huyo wa Pakistan aliyepewa kadi ya ukamataji wanyamapori 0016929 aliwahi kuwa na kesi nyingi za kujihusisha na ukamataji na usafirishaji wa wanyamapori hao kinyume na sheria,” alisema.
Kutokana na hali hiyo, alisema kamati hiyo imeshashauri Tarimo, Ahmed na wengine waliohusika katika sakata hilo wachukuliwe hatua stahiki.


Hata hivyo, kamati ilieleza kukabiliwa na changamoto ya kukosa ushirikiano kutoka wizarani hasa walipohitaji baadhi ya nyaraka muhimu kama barua halisi ya Jungle International kuomba kupatiwa wanyama na barua halisi ya serikali ya Jiji la Karachi kuomba kupatiwa tembo wanne na kumtambulisha Ahmed kama mwakilishi wake kwa Idara ya Wanyamapori nchini.
Zitto alisema kuwa Mlima Kagulu uliokuwa unamilikiwa na Shirika la Madini (Stamico) ulimilikishwa kwa Tanpower Resource kwa maagizo ya aliyekuwa Waziri wa Nishati wa wakati huo ambaye pamoja na kutomtaja jina lakini alikuwa ni Daniel Yona.
Zitto alisema kuwa Mlima Kagulu uliokuwa unamilikiwa na Shirika la Madini (Stamico) ulimilikishwa kwa Tanpower Resource kwa maagizo ya aliyekuwa Waziri wa Nishati wa wakati huo ambaye pamoja na kutomtaja jina lakini alikuwa ni Daniel Yona.
Alisema kampuni hiyo haikufuata utaratibu wa kumilikishwa mlima huo kwa mwekezaji mwingine, wakati imeingizia madeni makubwa serikali yafikiayo sh bilioni 33 ambazo zilikopwa na wawekezaji hao kutoka benki mbalimbali ambapo kwa sasa zinalipwa na serikali.
Zitto aliongeza kuwa licha ya hasara iliyosababishwa na Tanpower Resources, lakini serikali imelazimika kuilipa kampuni hiyo sh bilioni 9 kama ada ya kuendesha menejimenti ya mgodi huo jambo alilosema ni ukiukwaji mkubwa wa sheria.
“Kwa hali hii serikali iwajibike juu ya suala hili,” alisema Zitto kauli iliyomfanya Spika wa Bunge Anne Makinda kumtaka mbunge huyo kuwasilisha hoja hiyo kwa maandishi ili serikali kwa hoja yake ilikuwa nzito na ambayo lazima serikali itoa maelezo.
Wabunge wamtetea Waziri Nyalandu
KATIKA hatua isiyokuwa ya kawaida baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri wamemuunga mkono Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Lazaro Nyalandu, kuhusu sakata la Shirika la Viwango Nchini TBS.
Aidha wabunge hao wameshauri kwamba hoja inayoendelea hivi sasa kuhusu taarifa ya utendaji ya TBS na mapungufu yake isitumike vibaya kuwahujumu wanasiasa wengine badala yake wanaohusika wanapaswa kuwajibishwa kwa mujibu wa mapendekezo yaliyopo.
Wakizungumza katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima nje ya viwanja vya Bunge mjini hapa wabunge hao walisema taarifa hizo zinapaswa kufanyiwa kazi kikamilifu kwani zinaweza kuwaweka baadhi ya wanasiasa wakiwamo mawaziri katika hali tete.
“Tunaelewa kwamba katika hili ni nani anayetakiwa kuwajibishwa, lakini kumekuwa na maoni tofauti ambayo kwa utashi wa kawaida wa kisiasa, wanafanyiwa fitina ili kumshawishi Mheshimiwa Rais kuwaondoa,” alisema mmoja wa wabunge hao kutoka kanda ya ziwa.
Wabunge hao ambao waliomba majina yao yasitajwe gazetini walisema mapendekezo yaliyotolewa na kamati ya Wabunge wa CCM hayakuwataja baadhi ya mawaziri, lakini wameshangazwa kuona majina yao yakiunganishwa katika sakata hilo hatua ambayo inaweza kutafsiriwa vibaya na jamii.
“Tumekuwa katika vikao vya chama na mapendekezo yalikuwa ya wazi, hivyo haikuwa hoja ya msingi kuingiza majina ya baadhi ya mawaziri na tunadhani kwamba hatua hii inafanywa kwa makusudi na wala sio bahati mbaya,” alisema mbunge mwingine.
Mbunge huyo alisema binafsi hatoi maoni yake kwa nia ya kumtetea Naibu Waziri Nyalandu, bali anafanya hivyo ili kuonyesha uzalendo kwa taifa hili na kama kuna makosa mengine ameyafanya, anaweza kuwajibishwa lakini sio kwa hilo la TBS.
Kwa mujibu wa wabunge hao, kamati ya Bunge pamoja na ile ya CCM ilitoa ushauri kwamba Waziri wa Viwanda na Biashara Cyril Chami awajibishwe kutokana na kushindwa kuchukua hatua kulingana na mamlaka aliyopewa na sheria.
Walisema kwamba mfumo wa utendaji katika idara za serikali unatambua nafasi ya Waziri na Naibu Waziri, hivyo suala linalomhusu waziri kamwe haliwezi kuchukua nafasi ya Naibu Waziri kutokana na uzito wa jambo husika.
“Ndio maana hata katika vikao vya uchambuzi wa taarifa za kamati, suala hili tumelisemea kwa kiasi kikubwa na kuweka msimamo kuwa anayetakiwa kuwajibika kwa kushindwa kulifanyia maamuzi ni Waziri mwenye dhamana na wala sio mtu mwingine,” alisema mbunge mwingine.
Mbunge huyo alisema ikiwa Watanzania wataendelea kupewa taarifa zisizo za kweli watashindwa kuiamini serikali, lakini pia watakuwa wamewekewa chuki za kisiasa moyoni dhidi ya baadhi ya mawaziri waliopo madarakani na kusema mfumo wa sasa unaingilia mamlaka nyingine za uteuzi kwa mujibu wa Katiba ya nchi.
“Tunakubali kwamba kuna baadhi ya wanasiasa wameshindwa kusimamia majukumu waliyopewa na Rais ama wamechoka au kulewa madaraka, hivyo ni muhimu kuchukuliwa hatua kali ili iwe fundisho kwa wengine wasioweza kufanya majukumu kwa mujibu wa taratibu zao,” alisema mbunge mwingine.
Hata hivyo, Waziri wa Viwanda na Biashara Cyril Chami, alisema kwa sasa hawezi kusema chochote kwa vile yupo kwenye msiba mjini Moshi.
“Samahani ndugu yangu, niko Moshi nimefiwa, hivyo sitakuwa katika nafasi nzuri ya kulizungumzia suala hilo, nakuomba ufanye subira kwani Waziri Mkuu anaweza kulitolea ufafanuzi suala hilo wiki hii,” alisema Chami.
Wabunge bado walia na mawaziri
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu ‘Sugu’, alisema taifa limepoteza fedha nyingi kutokana na uzembe wa mawaziri na kuhoji wanyama kama twiga waliosafirishwa walitumia usafiri gani.
“Hata kama mnasema hamtajiuzulu, hiki kimbunga ni lazima king’oe bati ambalo ni Mheshimiwa Pinda. Huu sio upepo ni dhoruba nasema kama mmeshindwa achieni ngazi sisi tushike madaraka, kama tunatoa bajeti mbadala na inakubaliwa kwa asilimia 99 tunaweza,” alisema.
Aliongeza kuwa hata CCM ikiwa chama pinzani hawataki kiwe legelege na kuongeza kuwa ndiyo maana wakati huu wanawanyoosha.
Pamoja na hayo, Sugu alisema endapo wangekuwa wanafuata hasira za wananchi, viti vya bungeni vingekuwa vimeshang’olewa siku nyingi.
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), alisema mawaziri wanaogoma kujiuzulu ni lazima wajiuzulu, kwani lazima inakuja tsumani katika suala hilo.
Alisema ni mambo ya kushangaza kila mwaka yanazungumza masuala hayohayo, lakini hakuna kinachobadilika na kuongeza kuwa vizazi vijavyo vitakuja kuwalaumu.
“Wabunge tunapoibua masuala haya naona mawaziri wanaona ni mzaha, kwani mjadala uliopoanza Waziri Maige ametoka nje ya ukumbi wa Bunge.
“Kule KIA (Kilimanjaro International Airport) vijana wanalalamika kuwa kuna baadhi ya watu wanaokuja kugongewa passport zao huku wenyewe wakiwa kwenye ndege,” alisema.
Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (NCCR-Mageuzi), alisema kutokana na hali inayoendelea serikalini ndiyo maana wanawataka mawaziri hao kujiuzulu kutokana na kuihujumu nchi.
Alisema ni jambo la kushangaza kampuni kupatiwa vibali bila kuomba na kuongeza kuwa viongozi wa CCM ndio wanaoiangusha serikali yao.
“Jamani hii nchi ni ya aina gani, ni kitu gani mnafanya? Tuwaelewaje? Hivi mnatuona wapinzani ni nyanya mbichi?...mheshimiwa Spika funga mlango tushikane mashati,” alisema.


Zitto awashukia Ngeleja, Malima
Kwa upande wa Ngeleja, Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) Kabwe Zitto (CHADEMA) alimshambulia waziri huyo na Naibu wake Adamu Malima kwa madai ya kusema uongo kuhusiana na uwekezaji katika mgodi wa Kiwira.
Zitto akitoa taarifa kwa Bunge kutokana na jibu la Ngeleja aliyedai kuwa kampuni ya Tanpower Resources kwa sasa ni mfilisi baada ya kushindwa kuendeleza uwekezaji katika mgodi wa Kiwira na ikaurudisha serikalini na imelazimika kuhamisha umiliki wa Mlima Kagulu ambao unasadikiwa kuwa na mashapo yapatayo tani milioni 80 za makaa ya mawe kwenda kwa kampuni ya Tanzacoal kwa kufuata taratibu zote za kisheria.
Mlima huo wenye hazina kubwa ya makaa ya mawe ndiyo tegemeo la mwekezaji ambaye atamilikishwa Kiwira kuchimba makaa ya mawe kwa ajili ya kuzalisha megawati 400 za umeme.
Zitto alidai kuwa waziri huyo ndiye aliyeiagiza Stamico isiombe tena leseni ya kumiliki mlima huo wenye utajiri wa makaa ya mawe badala yake akaipa kampuni ya Tanpower Resources ambayo alikuwa na hisa nayo.
Source:Tanzania Daima at freemedia

Van Persie AMESHINDA MCHEZAJI WA MWAKA (PFA)

Van Persie (kulia)

Arsenal striker Robin van Persie has been named the Professional Footballers' Association Player of the Year.
The 28-year-old Holland international has scored 27 Barclays Premier League goals this season for Arsène Wenger's side - his most fruitful campaign for the Club - and was humbled to be recognised by his peers.
"If other people are saying it, it is special, but it is even more special if your opponents are saying it," he told Press Association Sport.
"It is very special because you are playing against them week in week out and every single player does everything to win. In the end, if they make up their minds that I am the best player it is a big honour."
Van Persie may have picked up the top individual honour but he was quick to point out it would not have been possible without his Arsenal team-mates.
"Without them I could not have achieved it," he said.
"For example Theo Walcott, he has given me more than 12 assists and I do really appreciate that."
Van Persie was utilised mainly as a second striker, and occasionally out on the wing, in the early stages of his Gunners career after being signed by Wenger from Feyenoord in 2004.
But he has flourished since switching to the centre-forward role - despite initially not having been convinced he could make the transition.
"Now I am [confident]," he said. "To be fair, when I first went there I wasn't really as confident and I wasn't really sure I could do it. It took a bit of time but after a couple of months a slowly realised I could do a good job there."
The Young Player of the Year award went to Tottenham and England full back Kyle Walker.
The 21-year-old Spurs defender beat the likes of Alex Oxlade-Chamberlain, Sergio Aguero and Danny Welbeck to win the trophy and came as quite a surprise to the former Sheffield United man.
"I was a bit surprised because defenders don't normally get these awards and get the limelight as much as the centre forwards," he said.

"If you look at the people I was in with then it is a great honour to get the award and hopefully there is more to come.

"It is always an honour to be selected by the people you play against and, like I say, hopefully I can get a few more of these and some medals with Tottenham along the way."

Both players were also selected in the Premier League's Team of the Year. Van Persie was the only Arsenal player present whereas Walker was one of three Spurs men, with Scott Parker and Gareth Bale also included.

The PFA Merit award was presented to Preston defender Graham Alexander in recognition of his services to the game, dating back to his debut as a Scunthorpe player in 1991.

The Scotland international went on to play for Luton, Preston and Burnley before returning to Deepdale in 2011 and was humbled with the award of the trophy.

"To get recognition for what you have done in your career at any stage is great," he said.

"I'm coming towards the end of my playing career and I'm privileged to be recognised by the people who I have played against for the last 20-odd years."

Mawaziri wanaotakiwa kujiuzuru kutokana ubadhilifu wa mali ya UMMA


Kujiuzuru kwa mawaziri hao ni matokeo ya hoja ya mheshimiwa mbunge Zitto Kabwe ambae katika kikao kilichopita aliliomba bunge kupiga kura ya kutokuwana imani na waziri mkuu kwa kushindwa kuwadhibiti mawaziri wake na kuruhusu uzembe, ubadhirifu na ufisadi ndani ya serikali. Kat...ika maelezo yake mheshimiwa Zitto Kabwe aliwaomba wabunge kuweka itikadi za vyama vyao pembeni ili kuinusuru nchi na baada ya kikao cha bunge akaendesha kampeni ya kukusanyasaini za wabunge ili kutimiza masharti ya kanuni za bunge yanayotakiwa kufuatwa ili kuweza kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu.. YALIYOTOKEA J.mosi Mheshimiwa Naibu Spika, bila kumwajibisha Waziri Mkuu hawa Mawaziri waliotajwa hawatatoka na wasipotoka madudu haya yatarudia. Kwa hiyo Mbunge yoyote mwenye uchungu na ubadhirifu, Mbunge yoyote ambaye anakereka na watoto kwenye Jimbo lake kukaa chini, Mbunge yoyote anayekereka na madawa kuharibiwa na MSD na MSD kushindwa kupeleka madawa kwenye vijiji vyetu, nampa taarifa kwamba kuanzia kesho tunakusanya sahihi za Wabunge 70,ili siku ya Jumatatu tutoe hoja hapa Bungeni ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu. ( Makofi ) Mheshimiwa Naibu Spika, na kipindi hiki tunakitoa Mawaziri wote ambao wapo implicated kwenye taarifa hizi waweze kuona ama wao, au wamtoe rehani Waziri Mkuu. ( Makofi ) Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wabunge wote wenye uchungu kuanzia kesho tutakuwa pale mlangoni, sahihi zinazohitajika ni 70 tu, kwa ajili ya kuleta hapa Bungeni na Wabunge wanahitajika kupitisha hilo azimio ni nusu tu ya Wabunge, 50 plus one .Tukifanya hivyo tutakuwa tumewapa heshima wananchi wetu, wataona kweli tumewatendea haki badala ya kupiga kelele bila ya kuchukua action. ( Makofi ) Mawaziri saba waachia ngazi... Mhe. George Mkuchika Mawaziri saba wa serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania wameandika barua za kujiuzuru nafasi zao kufuatia tuhuma nzito za ubadhirifu wa mali ya umma zilizokuwa zikiwakabili baadhi ya mawaziri hao. KIKAO CHA DHARURA BAADA YA BUNGE Kujiuzuru kwa mawaziri hao kumefuatia kikao cha dharula kilichoitishwa na waziri mkuu mheshimiwa Mizengo Pinda muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao cha bunge mjini Dodoma. Mhe. Mizengo Pinda Waziri Mkuu mheshimiwa Mizengo Pinda yupo katika hatari ya kupoteza nafasi yake baada ya wabunge 75 kutia saini za kupendekeza kupigwa kura ya kutokuwa na imani nae. Majina ya mawaziri waliojiuzulu usiku wa jumamosi yametajwa hapo juu na picha zao kama zinavyoonekana.