Hii ni baada ya mechi iliyofanyika jana baada Simba kuipachika JKT Ruvu mabao matatu mtungi huku YANGA ikilala kwa KAGERA SUKARI
Wachezaji wa Simba wakishangilia juu ya ushindi wao |
Timu wa Wekundu wa Msimbazi, Simba SC jana imeendelea kujikita kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuirarua JKT Ruvu kwa mabao 3-0 kwenye mchezo uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar. Huko Bukoba mkoani Kagera, mahasimu wa Simba, Yanga SC wamelala kwa bao 1-0 kutoka kwa wenyeji Kagera Sugar, katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, basi hapo simba inazidi kujiahakikishia ubingwa kwa kuwa na pointi 50.