Hall, raia wa Uingereza, amesema watafanya kila linalowezekana kuchuana na Simba hadi hatua ya mwisho, ili waone kama watatwaa ubingwa au watashika nafasi ya pili.
“Ukiangalia tuna nafasi ya kutwaa ubingwa, tunatakiwa kushinda mechi zote tatu. Itategemea pia Simba itacheza vipi karata zake, tukishindwa basi angalau nafasi ya pili,” alisema Hall.
“Kila mchezaji anajua tuko katika nafasi gani, ubingwa au nafasi ya pili vyote vinawezekana na haitakuwa kazi rahisi.”
Hall alisema yupo kwenye maandalizi ya mechi yao dhidi Mtibwa Sugar, itakayochezwa kesho, ambayo inaweza kuwa na majibu sahihi.
Azam ipo katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 50.